Waziri wa Elimu Julius Ogamba amekanusha madai kwamba wanafunzi waliopata alama ya C+ mwaka uliopita hawatajiunga na vyuo vikuu.
Ogamba amesisitiza kuwa alama za chini za kujiunga na vyuo vikuu bado ni C+ ilivyotangazwa awali.
Ameongeza kuwa wanafunzi wote 246,391, waliopata alama ya C+ na zaidi katika mtihani wa kitaifa wa KCSE mwaka jana, watajiung na vyuo vikuu.
Waziri amefichua kuwa mtandao wa wanafunzi kuchagua kozi, KUCCPS utafunguliwa mwezi ujao.