Wanafunzi Nyandarua wahimizwa kufuatilia elimu jumuishi

Marion Bosire
3 Min Read

Mikakati finyu ya kifedha imeifanya serikali kusitasita kuidhinisha kuanzishwa kwa vyuo vikuu vipya, kwa mujibu wa Naibu Chansela wa Chuo Kikuu cha Nairobi – UoN Profesa Margaret Jesang Hutchinson.

Akihutubia kundi la kwanza la wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Nyandarua—ambacho kwa sasa kinasaidiwa na chuo kikuu cha Nairobi, Profesa Hutchinson alieleza kwamba serikali inakabiliwa na changamoto kubwa za kifedha, hali inayokwamisha kuanzishwa kwa vyuo vipya.

Alibainisha kuwa chuo hicho kikuu kinabadilisha mkondo wake wa kimkakati kutoka kutoa tu programu za kitaaluma hadi kulenga mahitaji na matarajio ya kimataifa.

Naibu Chansela huyo alihakikishia wanafunzi kwamba watapata fursa sawa na wenzao walioko katika mabewa mengine ya chuo kikuu cha Nairobi kote nchini.

Alisisitiza dhamira ya chuo hicho kuhakikisha taasisi hiyo mpya ina vifaa vya kutosha na kuweka mwanafunzi kama kitovu cha maamuzi yote.

“Tutahakikisha maktaba imejaa vitabu vya kutosha. Wanafunzi hapa watapokea huduma sawa na wenzao katika mabewa mengine ya UoN. Lengo letu ni kuwapatia elimu bora kabisa kutoka UoN. Ujasiriamali utaingizwa katika masomo yenu ili mhitimu mkijitambua katika nyanja mbalimbali za maisha,” alisema Hutchinson.

Aliwakanya wanafunzi pia dhidi ya matumizi mabaya ya mtandao, akionya kwamba shughuli nyingi zisizo na tija mitandaoni zinapoteza ndoto za vijana wengi.

Gavana wa Nyandarua, Kiarie Badilisha, alitafakari kuhusu safari ya kuanzishwa kwa chuo hicho, iliyoanza mwaka 2015 kwa kuundwa kwa kamati ya kiufundi.

“Hatua halisi ilianza mwaka 2022. Imekuwa safari ndefu na ya kimiujiza, na namshukuru aliyekuwa Naibu Chansela wa UoN, Profesa Stephen Kiama, aliyelisaidia wazo hili. Milango yote tuliyobisha ilifunguliwa. Hatua yetu inayofuata ni kuhamia katika Shule ya Upili ya Salient mwakani, ambapo tumepata ekari 100 za ardhi,” alisema.

Gavana Badilisha alielezea chuo hicho kama kutimia kwa ndoto ya muda mrefu.

Mkuu wa kwanza wa Chuo Kikuu cha Nyandarua, Profesa John Kimenju, alisema taasisi hiyo itajihusisha kikamilifu katika huduma kwa jamii kama njia ya kushukuru kwa usaidizi waliopata kutoka kwa wenyeji.

“Tutaanzisha mpango madhubuti wa ulezi ili kulea mashujaa wa kitaifa watakaokuwa mabingwa wa kimataifa. Utafiti wetu utalenga kuzalisha maarifa, teknolojia, na ubunifu utakaotatua changamoto za jamii moja kwa moja,” alisema Profesa Kimenju.

Chuo hicho kimeanza na vitivo vitatu na kinapanga kupanuka kadri miundombinu inavyoimarika.

Share This Article