Majirani Tanzania huenda wakawa miongoni mwa orodha mpya ya mataifa yanayotarajiwa kupigwa marufuku na kuwekewa vikwazo vya usafiri na Marekani.
Katika waraka uliodukuliwa, Tanzania imo kwenye orodha hiyo mpya pamoja na Angola, Misri, Ethiopia, Ivory Coast na Nigeria.
Mataifa mengine ni pamoja na Niger, Sao Tome and Principe, Senegal, South Sudan, Uganda, Zambia na Zimbabwe.
Nchi zitapewa muda wa siku 60 kushughulikia na kutatua masuala yatakayoibuliwa na Marekani; la sivyo, yatawekewa vikwazo vya kusafiri au kupigwa marufuku kwa raia wake kuingia Marekani na kwa mataifa washirika wa karibu wa Marekani.
Marekani ilipiga marufuku usafiri kwa raia wa mataifa ya Chad, Congo, Equatorial Guinea, Eritrea, Libya, Somalia, na Sudan huku Burundi, Sierra Leone na Togo yakiwekewa vikwazo.