Timu za taifa za Kenya za wachezaji saba upande kwa wanaume Shujaa na ile ya wanawake Lionesses ziko mjini Los Angeles,Marekani tayari kwa mechi za kuwania kupandishwa na kushushwa ngazi baina ya tarehe 3 na 4 mwezi huu.
Kenya imeratibiwa kupambana na Samoa Jumamosi hii kabla ya kuchuana na Ureno na Marekani Jumapili.
Kenya Lionesses itafungua kampeini zake dhidi ya Uhispania Jumamosi kabla ya kukumbuna na Brazil na Colombia.