Rais William Ruto amekutana na viongozi kadhaa kutoka barani Afrika kujadili mageuzi ya Umoja wa Afrika, AU.
Kwenye hotuba yake, Ruto alisema kuwa kikao hicho kiliafikiana kuimarisha utendakazi wa mahakama ya kisheria ya AU.
Aidha, viongozi hao walisema ipo haja ya umoja huo kuratibu upya mfumo wa kudumisha amani na kusuluhisha mizozo.
Ruto alielezea kutamaushwa kwake na hali ilivyo mjini Goma mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, na kusema wamepanga kikao na viongozi wengine kutoka Jumuiya ya Afrika Mashariki kesho kutwa, ili kujadiliana na Rais Paul Kagame wa Rwanda na pia Rais Felis Tshisekedi wa DRC jinsi ya kutafuta suluhu.
Viongozi waliohudhuria kongamano hilo ni pamoja na Marais Azali Assoumani wa Comoros, Général Umaro El Mokhtar Sissoco Embalo wa Guinea-Bissau, Taye Selassie kutoka Ethiopia, na John Dramani Mahama wa Ghana, pamoja na Rais wa Tume ya Umoja wa Afrika, Moussa Faki Mahamat.