Polisi wamepata mifugo 12 waliokuwa wameripotiwa kuibwa Juni 26, katika msitu wa Ndumuru.
Ng’ombe hao waliopatikana walikuwa wameripotiwa kuibwa Juni 26, katika kituo cha polisi cha Kangeta, kabla ya msako kuendeshwa na mifugo hao kupatikana Jumamosi Juni 28 .
Tyari ng’ombe hao wamekabidhiwa wamiliki katika kijiji cha Bullow eneo la Igembe North.
Polisi wameapa kuendeleza msako wa kukabiliana na wezi wa mifugo katika eneo hilo.