Maafisa wa polisi wamewakamata washukiwa wanane wa wizi wa kimabavu katika eneo la Tayari, kaunti ndogo ya Molo, kaunti ya Nakuru.
Wakati wa operesheni hiyo, polisi walipata simu za rununu, laini za simu, vitambulisho vya kitaifa na vipuri vya magari.
Yamkini maafisa wa polisi walitekeleza uvamizi huo baada ya kudokezewa na wananchi.