Mshukiwa Mkuu kwenye uvamizi wa hospitali ya Kitengela akamatwa

Tom Mathinji
1 Min Read
Mshukiwa wa uvamizi kwenye hospitali ya Kitengela akamatwa.

Maafisa wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI), wamemkamata mshukiwa anayehusishwa na uvamizi na uharibifu wa mali katika hospitali ya kaunti ndogo ya Kitengela  wakati wa maandamano ya Saba saba.

Elvis Otieno Owino, alitambuliwa na kamera za CCTV kuwa mmoja wa watu waliotekeleza mashambulizi dhidi ya hospitali hiyo.

Baada ya kukamatwa, Owino aliwaelekeza maafisa hao wa upelelezi nyumbani kwake huko Noonkopir,ambako  walipata kofia na jaketi ya rangi ya kijivu anazoaminika kuvalia wakati wa kisa hicho.

Anazuiliwa na polisi uchunguzi ukiendelea, huku makachero wakiwatafuta washukiwa zaidi waliovamia hospitali hiyo.

Kisa hicho kilitokea tarehe Julai 7,2025  jioni wakati kundi la wahuni lilipoishambulia hospitali hiyo.

Wahuni hao walitatiza huduma za matibabu  zikiwemo upasuaji uliokuwa ukiendelea wa kumsaidia mwanamke mmoja kujifungua, kuharibu vifaa katika chumba cha upasuaji na kuwasha moto kwenye lango la hospitali hiyo.

TAGGED:
Share This Article