Mkurugenzi wa mashtaka ya umma akariri kupigania haki za wanahabari nchini

Dismas Otuke
1 Min Read

Mkurugenzi Mkuu wa mashtaka ya umma Renson Mulele, amekariri kujitolea kwa afisi yale kupigania haki za wanahabari katika utendakazi wao.

Akiwahutubia wanahabari ,Mulele amesema afisi yake itaharakisha  kesi za uhalifu dhidi ya wanahabari,kuwalipa wanahabari wanaofichua maovu na kuhakikisha ulinzi wenye usawa pamoja kuandaa mafunzo ya pamoja kwa viongozi wa mashtaka,wanahabari na polisi.

Mulele ameyasema haya mapema Alhamisi alipokutana na viongozi wa chama cha wahariri wa vyombo vya habari nchini KEG.

 

Share This Article