Chama Cha Mapinduzi (CCM) nchini Tanzania kimemteua mwanawe Rais wa awamu ya tano Hayati John Pombe Magufuli, Jessica Magufuli, kugombea Ubunge wa Viti maalum kupitia kundi la UVCCM.
Aidha, CCM kimemteua Salma Kikwete, mkewe Rais mstaafu Jakaya Kikwete, kuwa mgombea pekee wa ubunge jimbo la Mchinga, mkoani Lindi.

Tanzania itashiriki uchaguzi wa udiwani, ubunge, na urais Oktoba 28 mwaka huu.