McCarthy ataja kikosi kwa mechi za mwisho kufuzu Kombe la Dunia

Dismas Otuke
1 Min Read

Kocha Mkuu wa Harambee Stars Benni McCarthy, ametaja kikosi kwa mechi mbili za mwisho za kundi F, kufuzu kwa fainali za Kombe la Dunia mwezi ujao ugenini.

McCarthy amewaita kikosini wachezaji wawili kwa mara ya kwanza akiwemo beki anayesakata soka nchini  Uingereza Vincent Harper  na mshambulizi Lawrence Okoth wa timu ya chipukizi chini ya umri wa miaka 20.

Kenya itamenyana na  Burundi tarehe 9 mwezi ujao mjini Bujumbura, kabla ya kufunga ratiba dhidi ya Ivory Coast siku 5 baadaye mjini Abidjan katika mechi za kundiF.

Harambee Stars  ni ya tano katika kundi hilo kwa alama 9.

Kikosi hicho kitaraipoti kambini mapema mwezi ujao kabla ya kikosi cha mwisho kutajwa.

Kikosi

Makipa

Faruk Shikhalo, Byrne Omondi, Brian Bwire

Mabeki

Manzur Suleiman, Vincent Harper, Sylvester Owino, Alphonce Omija, Collins Sichenje, Michael Kibwage, Ronney Onyango, Abud Omar, Daniel Sakari

Viungo

Alpha Onyango, Duke Abuya, Timothy Ouma, Ben Stanley, Marvin Nabwire, Austine Odhiambo

Wingá

William Lenkupae, Job Ochieng, Boniface Muchiri

Washambulizi
Michael Olunga, Ryan Ogam, Lawrence Okoth

 

 

Share This Article