Mabingwa wanaoondoka wa Ligi kuu ya Kenya Gor Mahia wametangaza kuandaa derby ya mashemeji dhidi ya watani wao AFC Leopards Jumatatu ijayo Juni 2 katika uwanja wa Raila Odinga kaunti ya Homa Bay.
AFC Leopards na Gor waliambulia sare tasa katika mkumbo wa kwanza uliopigwa uwanjani Nyayo Machi 30 mwaka huu.
Mechi hiyo ya raundi ya 33 hata hivyo haitakuwa na uzito kwani Gor, ambao wana uwezo finyu wa kutwaa ubingwa wa ligi Kuu wakihitaji kushinda mechi zote tatu na kutarajia Police FC, watapoteza mechi zao mbili za mwisho ili wahifadhi taji.
Gor watafunga msimu na Police FC Juni 15.
Mechi hiyo iliahirishwa awali kutokana na kukosa kwa uwanja.