Kwemoi na Krop wafuzu kwa Olimpiki

Dismas Otuke
0 Min Read

Ronald Kwemoi na Jacob Krop wamejikatia tiketi kwa michezo ya Olimpiki ,baada ya kumaliza katika nafasi za kwanza na pili za fainali ya mita 5,000 iliyoandaliwa mapema Jumamosi katika uwanja wa taifa wa Nyayo.

Kwemoi ameziparakasa mbio hizo za mizunguko 12 unusu kwa dakika 13 sekunde 27.20,akifuatwa na Krop kwa dakika  13 sekunde 27.54,huku Edwin Kurgat akiambulia nafasi ya tatu.

 

Share This Article