Kombe UEFA  Champions League liko Nairobi

Dismas Otuke
1 Min Read

Kombe la kifahari la  Ligi ya  bingwa barani Ulaya (UEFA  Champions League) limewasilishwa  Kenya katika ziara  amabyo pia litazungushwa katika  mataifa tano ya  Vietnam, Indonesia, Afrika Kusini, Zambia na Kenya.

Ziara hiyo inayofadhiliwa na kampuni ya Heinken inaongozwa na aliyekuwa kiungo mkabaji wa  klabu za Manchester United na Bayern Munich -Bastian Schweinsteiger,na  inalenga kuwapa wapenzi wa soka nchini fursa ya kutazama kombe hilo .

Mapema Ijumaa Schweinsteiger, aliyeshinda taji hiyo mwaka  2013 na Bayern Munich, aliwasilisha kombe kwa wanahabari katika hoteli ya Serena jijini Nairobi..

Baadaye Leo, kombe  hilo liliwasilishwa kwa Rais William Ruto katika ikulu ya Nairobi kwenye hafla iliyohudhuriwa na maafisa wa wizara ya michezo, shirikisho la kandanda nchini ( FKF), Kenya wines Agency limited ( KWAL), Kampuni ya Heineken na UEFA.

Kesho jumamosi, Heineken na FKF wataandaa kikao na  vigogo wa kabumbu humu nchini watakaotangamana na Schweinsteiger.

Aidha  Mashabiki 700 wa kwanza watapata fursa ya kutazama na kupiga picha na kombe hilo.

Ziara hii amabayo ilianza tarehe saba Aprili nchini Vietnam, na inakamilikia hapa nchini,na inalenga  kuwapa  mashabiki na wadau wa soka fursa ya kutangamana, kabla ya fainali ya Makala ya mwaka  huu itakayogaragazwa ugani Alianz Arena, nchini Ujerumani tarehe 31 mwezi huu.

Share This Article