Kipute cha WAFCON charejea leo kwa robo fainali

Baadaye, saa nne usiku katika uchanjaa wa Olympique de Rabat, wenyeji Morocco watakabana koo na Mali.

Dismas Otuke
1 Min Read
Racheal Kundananji of Zambia celebrates goal with teammates during the 2024 Women's Africa Cup of Nations Final between Morocco and Zambia at the Olympic Stadium in Rabat, Morocco on 5 July 2025 ©Samuel Shivambu/BackpagePix

Kindumbwendumbwe cha kombe la bara Afrika kwa wanawake, WAFCON kitarejea nchini Morocco kwa mechi za robo fainali.

Mabingwa mara tisa Nigeria watafungua dimba dhidi ya Zambia katika mechi inayotazamiwa kuwa moto wa kuotea mbali kuanzia saa moja usiku katika uwanja wa Larbi Zaouli, mjini Casablanca.

Baadaye, saa nne usiku katika uchanjaa wa Olympique de Rabat, wenyeji Morocco watakabana koo na Mali.

Mechi mbili za awamu ya nane bora zitapigwa kesho Jumamosi, Algeria wakikumbana na Ghana saa moja usiku, huku mabingwa watetezi Afrika Kusini, ukipenda Banyana Banyana, wakimaliza udhia dhidi ya Senegal.

Share This Article