Kindumbwendumbwe cha Kombe la Dunia baina ya vilabu kitatarejea leo kwa mechi za robo fainali baada ya mapumziko ya siku moja.
Fluminense ya Brazil, watakumbana na miamba wa Saudi Arabia Al Hilal, kuanzia saa nne usiku katika uwnaja wa Camping World mjini Orlando.
Mapema kesho waakilishi wengine wa Brazil, Palmeiras watapimana ubabe na Chelsea ya Uingereza saa kumi alfajiri Lincoln Financial mjini Philadelphia.
Baadaye saa moja usiku mabinwga wa Ulaya PSG, watakuwa na mtihani mgumu dhidi ya Bayern Munich ya Ujerumani katika uchanjaa wa Mercedez Benz mjini Georgia .
Real Madrid kutoka Uhispania watashuka uwanjani Metlife mjini East Rutherford, kuanzia saa tano katika kwota fainali ya ya mwisho dhidi ya Borusia Dortmund.
Mabingwa wa kombe hilo watatuzwa donge nino la shilingi bilioni 16.256.