Kenya Pipeline walivuliwa ubingwa wa Zone 5 kwa wanawake baada ya kuambulia kichapo cha seti 3-1 kutoka kwa miamba wa Rwanda,Rwanda Patriotic Army (APR).
Vipusa wa KPC walinyakua seti ya kwanza alama 30-25,kabla ya kucharazwa seti tatu zilizofuatia 17-25,24-26 na 23-25.
Fainali hiyo iliandaliwa jana jioni katika ukumbi wa Lugogo jijini Kampala,Uganda.