Inter Milan kukwangurana na PSG fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya leo

Mabingwa wa leo watatia kibindoni dola milioni 27 huku watakaoshindwa wakienda nyumbani na dola milioni 20.5 za Marekani .

Dismas Otuke
1 Min Read
epa11865763 The UEFA Champions League trophy is pictured during the UEFA Champions League knockout phase play-off draw at the UEFA headquarters in Nyon, Switzerland, 31 January 2025. EPA/MARTIAL TREZZINI

Inter Milan ya Italia watapambana na PSG ya Ufaransa  leo usiku katika uchanjaa wa Alianz Arena mjini Munich, Ujerumani, kuwania kombe la Ligi ya Mabingwa barani Ulaya.

Fainali hiyo itakuwa ya kwanza chini ya mfumo mpya wa ligi ya Mabingwa ulioshirikisha timu 25 katika hatua ya Makundi.

Ili kufuzu kwa fainali Inter Milan waliibandua Uhispania Barcelona ya Uhispania mabao 4-3 ,huku PSG ikiwatema Arsenal mabao 3-1 katika hatua ya nusu fainali.

Mabingwa wa leo watatia kibindoni dola milioni 27 huku watakaoshindwa wakienda nyumbani na dola milioni 20.5 za Marekani .

Share This Article