Burna Boy kutumbuiza kwenye MadfunXperience jijini Nairobi

Tamasha hilo litakaloandaliwa katika Bustani za Uhuru tarehe 1 Machi linatarajiwa kuwa sherehe isiyosahaulika ya muziki wa Kiafrika.

Marion Bosire
1 Min Read

Tamasha la MadfunXperience linalosubiriwa kwa hamu kubwa litakalofanyika katika Bustani za Uhuru tarehe 1 Machi linatarajiwa kuwa sherehe isiyosahaulika ya muziki wa Kiafrika.

Burna Boy, nyota wa kimataifa, atakuwa mgeni mkuu wa usiku huu wa kihistoria wa maonyesho, na orodha ya wasanii inayojaa furaha ikiwemo msanii kutoka Kenya, Bensoul, nyota wa Afro-pop Charisma na DJ wa Amapiano kutoka Afrika Kusini, Virgo Deep.

Tukio hili linatarajiwa kutoa mchanganyiko wa aina mbalimbali za muziki, kutoka kwa nyimbo tamu za Bensoul hadi hisia za Afro-pop za Charisma, pamoja na midundo ya Amapiano ya Virgo Deep.

Kila msanii ataleta sauti yake ya kipekee, na usiku huo utakuwa mchanganyiko wa kusisimua wa uunganishaji wa muziki.

Usalama umepatiwa kipaumbele ambapo Kamanda wa Polisi wa kaunti ya Nairobi, Bi. Monica Kimani, ameahidi wahudhuriaji wa tamasha kwamba polisi watakuwepo kwa usalama wao.

Mashabiki wanaweza kutarajia ukaguzi wa usalama wa kipekee, ufuatiliaji wa ziada na usimamizi wa trafiki ili kuhakikisha uzoefu mzuri.

MadfunXperience ni zaidi ya tamasha ni sherehe ya sanaa ya Kiafrika.

Milango itafunguliwa saa tisa alasiri na kutakuwa na burudani usiku nzima, ikiwa ni pamoja na chakula, mitindo na tamaduni.

Tiketi zinapatikana kwenye Madfun.com. Usikose hii ni nafasi moja tu ya maisha!

Share This Article