Brazil yafuzu Kombe la Dunia kwa mara ya 23

Brazil wanajiunga  na mabingwa watetezi Argentina na Ecuador kutoka Amerika Kusini ,kujikatia tiketi kwa Kombe la Dunia mwaka ujao.

Dismas Otuke
0 Min Read

Mabingwa mara tano wa Dunia Brazil, walifuzu kwa fainali za 23  za mwaka ujao baada ya kuwapiga Paraguay goli moja kwa bila mapema leo.

Goli hilo na vijana wa Samba lilipachikwa kimiani na Vinicius Junior, mwishoni mwa kipindi cha kwanza  na kudumu hadi kipenga cha mwisho.

Brazil wanajiunga  na mabingwa watetezi Argentina na Ecuador kutoka Amerika Kusini ,kujikatia tiketi kwa Kombe la Dunia mwaka ujao.

 

 

Share This Article