Baba yake Jimmy Wanjigi afariki

Martin Mwanje
0 Min Read
Maina Wanjigi, mbunge wa zamani wa Kamukunji

Maina Wanjigi ambaye ni baba yake mfanyabiashara na mwanasiasa Jimmy Wanjigi ameaga dunia. 

Maina alifariki wakati akipokea matibabu katika hospitali moja jijini Nairobi.

Hadi kifo chake alikuwa na umri wa miaka 92.

Maina aliwahi kuhudumu kama mbunge wa Kamukunji na Waziri wa Kilimo, Ujenzi na Utalii.

Share This Article