Rais wa Madagascar asema atavunja serikali kufuatia maandamo ya Gen Z

Tom Mathinji
1 Min Read
Vijana Madagascar waandamana kulalamikia ukosefu wa maji na umeme kwa muda mrefu.

Rais wa Madagascar Andry Rajoelina, amesema atavunja serikali yake, kufuatia siku kadhaa za maandamano yanayoongozwa na vijana wanaolalamikia ukosefu wa maji na kukatika kwa umeme kwa muda mrefu.

“Tunakubali na tunaomba radhi kwani wanachama wa serikali hawajatekeleza majukumu waliyopewa,” alisema Rajoelina kwenye hotuba ya kitaifa iliyotangazwa na televisheni siku ya Jumatatu.

Maandamano hayo yanayoitwa Gen-Z yameshuhudia maelfu ya waandamanaji ambao wengi wao ni vijana wakiingia mitaani katika miji kote Madagascar tangu Alhamisi, chini ya kauli mbiu: “Maisha, bila kuteseka”.

Mkuu wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa amelaani “kikosi kisicho cha lazima” kinachotumiwa na vikosi vya usalama kutuliza machafuko, akisema kuwa watu wasiopungua 22 wameuawa na wengine 100 kujeruhiwa.

Share This Article