Rais wa Botswana Duma Boko ametangaza Septemba 29 mwaka huu kuwa siku ya mapumziko kusherehekea ushindi wa dhahabu ya Dunia na timu ya wanariadha wanne kupokezana kijiti kwa wanaume.
Timu hiyo iliandikisha historia katika mashindano ya Riadha Ulimwenguni iliponyakua dhahabu hiyo katika siku ya mwisho jana Jumapili, ikiwa mara ya kwanza taifa la Afrika kutawazwa mabingwa katika fainali hiyo.
Kikosi cha Botswana katika fainali hiyo kiliwashirikisha bingwa wa Olimpiki katika mita 200 Letsile Tebogho, bingwa wa dunia wa mita 400 Collen Kibinatshipi na Bayapo Ndori.