Hamas imelaani uamuzi wa baraza la mawaziri la usalama la Israel wa kuchukua udhibiti wa mji wa Gaza na kuwahamisha wakazi wake kwa nguvu, na kuutaja kuwa “uhalifu kamili wa kivita” dhidi ya Wapalestina karibu milioni moja.
Katika taarifa yake, kundi hilo liliishutumu serikali ya Waziri Mkuu Benjamin Netanyahu kwa kutekeleza kile ilichoita “usafishaji wa kikabila” na kupuuza hatima ya mateka wa Israel kwa kupanua zaidi vita.
Ilisema hatua hiyo inaelezea kujiondoa kwa Israel katika duru ya hivi punde zaidi ya mazungumzo ya kusitisha mapigano, ambayo Hamas ilisema ilikuwa karibu kufikia makubaliano juu ya mapatano na kubadilishana mateka.
Hamas ilisema imeonyesha “kubadilika na kuwa chanya” katika majadiliano na wapatanishi wa Qatar na Misri na imesalia wazi kwa makubaliano kamili ya kuwaachilia mateka wote wa Israeli kwa kubadilishana na kumaliza vita na kuondoa vikosi vya Israeli.
Kundi hilo lilionya kuwa mpango wa Israel “hautakuwa sana na matembezi katika bustani” na utakabiliwa na upinzani mkali.
Pia imeituhumu marekani kwa “kuwajibika kikamilifu” kwa kutoa msaada wa kisiasa na kijeshi kwa Israeli, na ilihimiza Umaoja wa Mataifa na mahakama za kimataifa kuchukua hatua kusitisha mpango huo.