Kikosi cha Harambee Stars kwa CHAN chatajwa

Kiranja wa kikosi atakuwa Aboud Omar akisaidiwa na Daniel Sakari na Alphone Omija.

Dismas Otuke
1 Min Read

Kocha mkuu wa timu ya taifa Harambee Stars, Benni McCarthy, ametaja kikosi cha mwisho cha wanandinga 25 watakaoshiriki fainali za kombe la CHAN mwezi ujao.

McCarthy ameajumuisha wachezaji wenye tajiriba na chipukizi huku Kenya ikishiriki fainali za CHAN kwa mara ya kwanza.

Fainali za CHAN zitaandaliwa kwa pamoja na Kenya, Uganda na Tanzania pamoja na Zanzibar kati ya Agosti 2 na 30 mwaka huu.

Makipa

Faruk Shikhalo, Byrne Omondi, Sebastian Wekesa

Mabeki

Siraj Mohammed, Manzur Suleiman, Pamba Swaleh, Abud Omar, Alphonce Omija, Sylvester Owino, Mike Kibwage, Daniel Sakari, Lewis Bandi, Kevin Okumu

Viungo

Brian Musa, Alpha Onyango, Austin Odhiambo, Ben Stanley, Marvin Nabwire

Washambulizi

Mohammed Bajaber, Boniface Muchiri, David Sakwa, Ryan Ogam, Masoud Juma, Austin Odongo, Felix Oluoch

Kiranja wa kikosi atakuwa Aboud Omar akisaidiwa na Daniel Sakari na Alphone Omija.

Kenya imejumuishwa kundi A pamoja na miamba Morocco, DR Congo, Zambia na Angola, huku wakifungua dimba dhidi ya DRC tarehe 3 mwezi ujao ugani Kasarani.

Share This Article