Wakenya waonywa dhidi ya kuwatisha maafisa wa polisi

Tom Mathinji
1 Min Read
Rais William Ruto

Rais William Ruto ametoa wito kwa wananchi kuheshimu  na kushirikiana na huduma ya taifa  ya polisi kabla ya maandamano ya vijana  ya   kuadhimisha mwaka mmoja tangu  maandamano ya vijana wa kizazi cha  Gen Z kushuhudiwa nchini.

Rais  Ruto aliwaonya wahalifu  dhidi ya kuwatishia au kuwashambulia maafisa wa polisi.

Akiongea  katika Ikulu ya Nairobi wakati wa dhifa ya kiamsha kinywa iliyoandaliwa kwa heshima ya timu za Kenya Police FC na Kenya Police Bullets kwa kushinda taji za Ligi Kuu ya FKF mwaka huu, kiongozi wa taifa  alisema serikali yake itaendelea kuwaunga mkono maafisa wa usalama waliojitolea kulinda maisha na mali ya Wa-Kenya.

“Tutawaunga mkono maafisa wa polisi, wao ni nguzo muhimu kwa udhabiti na ustawi wa taifa hili,” alisema Rais Ruto.

Alisema bila amani na usalama, nchi hii haitaendelea. Rais  Ruto alisema vitengo vya usalama  vinahitaji usaidizi wa kutosha ili kulinda  taifa hili.

TAGGED:
Share This Article