Miano atoa hakikisho la serikali kukamilisha miradi ya maendeleo Nyandarua

Dismas Otuke
1 Min Read

Waziri wa Utalii Rebecca Miano amekariri kujitolea kwa serikali kukamilisha miradi ya maendeleo  iliyoanzishwa katika kaunti ya Nyandarua.

Miano alisema haya Jumatatu alipohudhuria mazishi ya Mama Jane Wangari  eneo bunge la Ndaragwa, akisisitiza kuwa miradi hiyo itainua hadhi ya wakazi wa Nyandarua itakapokamilika.

Baadhi ya miradi hiyo ni ujenzi wa masoko ya kisasa, upatikanaji wa maji safi, uunganishaji wa umeme na kuboresha taasisi za elimu na vituo vya afya.

Share This Article