Sunderland yaipiga Sheffield United na kurejea Ligi kuu Uingereza baada ya miaka minane

Tom Watson alipachika kimiani bao la ushindi katika sekunde za mwisho na kuwanyanyua mashabiki kwa sherehe za kina aina .

Dismas Otuke
1 Min Read
Soccer Football - Championship - Play-Off Final - Sheffield United v Sunderland - Wembley Stadium, London, Britain - May 24, 2025 Sunderland's Daniel Ballard lifts the trophy as he celebrates with teammates Action Images via Reuters/Matthew Childs EDITORIAL USE ONLY. NO USE WITH UNAUTHORIZED AUDIO, VIDEO, DATA, FIXTURE LISTS, CLUB/LEAGUE LOGOS OR 'LIVE' SERVICES. ONLINE IN-MATCH USE LIMITED TO 120 IMAGES, NO VIDEO EMULATION. NO USE IN BETTING, GAMES OR SINGLE CLUB/LEAGUE/PLAYER PUBLICATIONS. PLEASE CONTACT

Sunderland imewalemea Sheffield United mabao 2-1 kwenye fainali ya kupandishwa ngazi hadi EPL iliyochezwa Jumamosi jioni katika uwanja wa Wembley, wakirejea ligini baada ya subira ya miaka minane na ushindi wa kwanza wa mechi hiyo ya mchujo baada ya kushindwa mara tano.

Sheffield United, waliomaliza katika nafasi ya tatu kwenye ligi ya Championship walichukua uongozi kunako dakika ya 25 kupitia kwa Tyrese Campbell,kabla ya Patrick Roberts kusawazisha dakika 15, kabla ya kipenga cha mwisho.

Tom Watson alipachika kimiani bao la ushindi katika sekunde za mwisho na kuwanyanyua mashabiki kwa sherehe za kina aina .

Sunderland maarufu kama Black Cats wamerejea ligini kwa mara ya kwanza tangu walipushwa daraja msimu wa mwaka 2016/2017.

Share This Article