Katibu Omollo akagua miradi ya maendeleo Kuria

Dismas Otuke
1 Min Read

Katibu katika Wizara ya Usalama wa Taifa Dkt. Raymond Omollo ameongoza shughuli ya kukagua miradi ya maendeleo inayotekelezwa na serikali kuu  katika eneo la Kuria.

Miradi hiyo ni pamoja na ule wa maji wa Kegonga eneo la Nyamache unaolenga kutoa maji safi kwa matumizi ya wakazi na ujenzi wa barabara ya Taranganya-Senta-Ntimaru-Nyamtiro OSBP-Kegonga-Kugitimo-Loliondo, ambayo itafungua fursa za kibiashara katika eneo hilo.

Aidha, Katibu huyo amefungua rasmi mradi wa usambazaji maji wa Kebaroti kwa ushirikiano na mamlaka ya maendeleo ya maziwa.

Omollo alifanya ukaguzi huo akiandamana na Gavana wa Migori Ochilo Ayacko, Seneta Eddy Oketch, mbunge wa Suna Magharibi Peter Masara, na mwenzake wa Kuria Mashariki Kitayama Maisori.

 

Share This Article