Friday, 13 Feb 2026

Welcome to the official Kenya Broadcasting Corporation (KBC) News YouTube channel.

 
Explore Now
KBC Swahili
  • Kimataifa
    • Vipindi
    • Habari Kuu
    • Taifa
  • Biashara
  • Burudani
  • Kaunti
  • Michezo
  • Videos
  • Paris Olympics 2024
  • Back to KBC
  • Kimataifa
  • Taifa
  • Habari Kuu
  • Michezo
  • Kaunti
  • Burudani
  • Vipindi
  • Biashara
  • Habari za Hivi Punde
  • Makala
KBC SwahiliKBC Swahili
Font ResizerAa
  • Kimataifa
  • Biashara
  • Burudani
  • Kaunti
  • Michezo
  • Videos
  • Paris Olympics 2024
  • Back to KBC
Search
  • Kimataifa
    • Vipindi
    • Habari Kuu
    • Taifa
  • Biashara
  • Burudani
  • Kaunti
  • Michezo
  • Videos
  • Paris Olympics 2024
  • Back to KBC
Have an existing account? Sign In
Follow US
© 2022 Foxiz News Network. Ruby Design Company. All Rights Reserved.
Burudani

Kanye West afuta akaunti yake ya mtandao wa X

Aliafikia hatua hiyo baada ya kuchapisha maneno kadhaa yanayoashiria chuki dhidi ya Wayahudi na wengine.

Marion Bosire
February 10, 2025 8:40 am
By Marion Bosire
Share
2 Min Read
SHARE

Mwanamuziki Kanye West amefuta akaunti yake ya mtandao wa X baada ya kuchapisha maneno kadhaa yanayoashiria chuki dhidi ya Wayahudi.

Awali, usimamizi wa mtandao wa X ulikuwa umeweka onyo la maudhui ya kutiliwa shaka kwenye akaunti hiyo ya Kanye.

Kanye alianza kuchapisha maneno hayo ya kusikitisha Ijumaa Februari 7, 2025 ambapo aliandika maneno kama vile kukiri kuwa mwanachama wa Nazi.

Aliandika pia kwamba haamini yeyote ambaye ni Myahudi na kwamba aliandika maneno hayo akiwa hajanywa pombe hata kidogo.

West aliyebadili jina na kuwa Ye mwaka 2022, aliendelea kuchapisha taarifa zisizo nzuri hatua iliyosababisha watu kadhaa kama vile David Schwimmer kumtaka mmiliki wa X Elon Musk kumpiga Ye marufuku.

Schwimmer alisema kwamba Ye amerejelea hulka yake ya mwaka 2022 akisema kwamba hawawezi kumkomesha kusema anayoyasema lakini wanaweza kumnyima jukwaa la kutoa maoni yake.

Chameleone arejea nyumbani kutoka Marekani
Koffi Olomide apeleka burudani nchini Uganda
Embarambamba na Getumbe watakiwa kuondoa nyimbo zao “chafu” mitandaoni
Mwigizaji Charles Ouda afariki

Alishangaa ni kwa nini Kanye West ambaye ana wafuasi milioni 32.7 kwenye mtandao wa X idadi ambayo ni mara mbili ya idadi jumla ya wayahudi anakwazwa na uwepo wao.

Schwimmer ambaye ni mwigizaji anasema matamshi ya Ye yanasababisha uhasama halisi dhidi ya wayahudi na hajui ni lipi baya zaidi kuliko lingine kati ya aliyoyachapisha Kanye.

West alianza kudhihirisha hulka ya kutopendelea wayahudi Disemba mwaka 2022 wakati alisema kwamba anampenda Hitler katika mahojiano na Alex Jones kwenye kipindi show Infowars.

Usemi wa Ye ulisababisha kampuni kadhaa zilizokuwa zikishirikiana naye kama vile Adidas, GAP na Balenciaga zikomeshe mikataba na yeye.

TAGGED:Antisemitic postsDavid SchwimmerElon MuskKanye WestX Account
Share This Article
Email Copy Link Print
Previous Article Meneja wa Jux amtakia mema kwenye ndoa
Next Article Kenya kuimarisha zaidi ushirikiano na nchi za kigeni, aahidi Rais Ruto

You May also Like

Burudani

Don Richard asimulia kuhusu matatizo ya kiafya

July 6, 2025
Burudani

Mshukiwa wa wizi wa kazi za Beyonce akamatwa

September 17, 2025
Burudani

Zanie Brown adai tasnia ya muziki nchini Uganda inaendeshwa na nguvu za kiroho

April 21, 2025
Burudani

Cindy Sanyu afichua atakachofanya akistaafu

October 29, 2025
Show More
  • More News:
  • Kenya
  • William Ruto
  • CAF
  • Tanzania
  • President William Ruto
  • Uganda
  • DCI
  • FKF
  • Rais William Ruto
  • Nigeria
  • Israel
  • Raila Odinga
  • USA
  • Rigathi Gachagua
  • FIFA
  • Musalia Mudavadi
  • EACC
  • DRC
  • China
  • gaza
KBC Swahili

Information You Can Trust: Stay instantly connected with breaking stories and live updates. From politics and technology to entertainment and beyond, we provide real-time coverage you can rely on, making us your dependable source for 24/7 news.

Youtube Medium Rss

About Company

  • Contact Us
  • Advertise with US
  • Complaint
  • Privacy Policy
  • Cookie Policy
  • Submit a Tip

Real-time Updates on the Latest Stories!

© Kbc Swahili.  All Rights Reserved. 2025

Welcome to Foxiz
Username or Email Address
Password

Lost your password?