Katibu wa Elimu ya msingi Belio Kipsang ameonya kuwa huenda mitihani ya kitaifa ikaathiriwa vibaya, kutokana na hatua ya serikali ya kupunguza bajeti ya wizara hiyo.
Kipsang amesema watahiniwa wapatao milioni 2.3 wanaotazamiwa kukalia mitihani ya kitaifa mwaka huu huenda wakaathiriwa na kupunguzwa kwa bajeti ambayo itavuruga mchakato mzima wa mitihani ya kitaifa.
Serikali imekata shilingi bilioni 14.9 za wizara ya elimu zikiwemo bilioni 8 za matumizi ya kila siku na nyingine bilioni 6.9 za kugharimia maendeleo katika wizara hiyo huenda kukatatiza utoaji huduma.
Kulingana na agizo hilo pia mpngp wa lishe shuleni ambao ulikuwa umetengewa shilingi bilioni tatu utaathiriwa baada ya bajeti yake kuondolewa na kuelekezwa kwingine.