Ruto kufanya kikao na Vijana wa Gen Z kupitia mtandao wa X- Space Ijumaa

Dismas Otuke
1 Min Read

Rais William Ruto anatarajiwa kukutana na vijana wa Gen Z kupitia  kwa mtandao wa X-Space, ili kujadili maswala yaliyoibuliwa na vijana hao wakati wa maandamani ya kitaifa yaliyodumu kwa majuma mawili.

Kikao hicho ambacho pia kitahudhuriwa na baraza zima la Mawaziri  kimeratibiwa kuanza saa nane adhuhuri na kukamilika saa kumi na moja jioni.

Itakuwa ni mara ya kwanza tangu kuanza kwa maandamano ya kupinga mswada wa fedha yaliyoongozwa na vijana hao.

Vijana hao walilazimika kufutilia mbali maandamano ya jana baada ya shughuli hiyo kuingiliwa na magenge ya majambazi ambayo yamekuwa yakipora mali  na kusababisha uharibifu .

Share This Article